Saturday, March 30, 2013

MATESO YA BWANA YESU

 TUMSIFU YESU KRISTU !

SISI SOTE TU WADHAIFU, TUMWOMBE MKOMBOZI WETU YESU KRISTU ATUJALIA NGUVU YA KIROHO ILI TUWEZE KUSHINDA MAOVU YOTE KATIKA MAISHA YETU, TUMWOMBE MFALME ATUJALIE UJASILI WA KIROHO ILI TUWEZE KUSEMA  HAPANA PALE SHERIA ZA NCHI ZINAPOPINDISHWA KWA MAKUSUDI KWA MANUFAA YA WACHACHE.

TUSEME HAPANA PALE VIONGOZI WETU WASIPOWAJIBIKA IPASAVYO KWA WANANCHI .

TUSEME HAPANA PALE VIONGOZI WETU WANAPOTISHWA ILI WASIKAMILISHE MAANGIZO YA BWANA WETU YESU KRISTU YA KUTANGAZA INJILI KWA WATU WOTE HADI MWISHO WA DUNIA.

TUSEME HAPANA PALE WATU WACHACHE WANAPOTAKA KUHALALISHA USHOGA .

TUSEME HAPANA PALE  VIONGOZI WETU WASIPOLINDA MALI ASILI ZA NCHI

TUSEME HAPANA UASHERATI !

TUSEME HAPANA KUSEMA UONGO !

TUSEME HAPANA KUIBA !

TUSEME HAPANA UVIVU ! ADUI WA MAENDELEO.

TUSEME HAPANA KUUWA !

NDUGU WAPENDWA KATIKA KRISTO TUONGOZWE NA ROHO MTAKATIFU NA HAKIKA TUTASHINDA VITA HIVI VYA KIROHO NA BILA SHAKA TUTAWEZA KUSEMA HAPANA ! HAPANA !HAPANA ! HAPANA ! NA MUNGU WETU WA MAJESHI ATATUONGOZA DAIMA.


AMANI NA SALAMA

No comments:

Post a Comment