Tuesday, April 3, 2012

PAPA ATOBOA SIRI YA ROZARI

397035_Shop Hot & Cheap Cell Phones With Free Shipping 250*250 Banner

Papa atoboa siri ya Rozari
l Alipigwa risasi Siku ya Bikira Maria wa Fatima
l Aliitolea Tanzania kwa Bikira Maria
          
VATICAN CITY

BABA Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili,ametoboa siri ya yeye kuhimiza matumizi ya Sala ya Rozari Takatifu ya Bikira Maria.
Akizungumza kwa waamini wa waliokusanyika katika Viwanja vya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro hivi karibuni, Baba Mtakatifu aliwahimiza Wakatoliki na watu wengine wanaosali Sala ya Rozari Takatifu, kuwa rozali inajumuisha njia bora za kukuza majitoleo ya kutafakari uso wa Kristo.
“Sababu muhimu ya kupendekeza tena kusali Rozari, ni ukweli kwamba inajumuisha njia bora za kukuza majitoleo ya kutafakari uso wa Kristo miongoni mwa waamini, jambo nililoliomba kufuatia Jubilei Kuu ya mwaka 2000,” alisema Baba Mtakatifu.
Akaongeza, “Bikira Maria ni mfano mkubwa wa tafakari ya Kikristo,” alieleza Papa akikumbuka maudhui ya barua yake ya kitume “Rosarium Virginis Mariae.”
“Tangu kuchukuliwa mimba kwa Kristo mpaka ufufuko na kupaa kwake mbinguni, Mama yake aliendelea kuelekeza moyo wake usio na doa kwa Mwanae wa Kimungu: tafakari ya ajabu, inayopenya mioyo, ya huzuni na yenye kung’ara,” alisisitiza.
“Ni katika mtazamo huu wa Ki-Maria, uliojaa imani na upendo, Mkristo na Jumuiya ya Kanisa, hufanya sala yao wakati wanaposali Rozari,” alisema Papa.
Alisema, hiyo ndiyo sababu ya yeye kupendekeza kuongezwa kwa Mafumbo ya Nuru katika Rozari, yanayohusu maisha na kazi za Yesu.
Katika KIONGOZI toleo lililopita, tuliripoti kuwa katika Maadhimisho ya Miaka 24 ya Upapa, Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili, alitangaza Mwaka wa Rozari na kupendekeza Mafumbo ya Nuru kuongezwa katika sala hiyo.
Historia ya maisha ya Papa Yohane Paulo wa Pili inaonyesha wazi Ibada kubwa aliyonayo yeye binafsi kwa Mama Bikira Maria. Tangu aliposimikwa kuwa Baba Mtakatifu ,aliutolea utume wake chini ya maombezi ya Bikira Maria,ndiyo maana hata nembo yake ina herufi’M’ ikimanisha ‘Matoleo maalumu kwa Bikira Maria’.
Katika  tukio lisilo la kawaida la jaribio la kumuua,lililofanyika Mei 13 mwaka 1981 na Mehmet Ali Agea (23) raia wa Uturuki,jaribio hilo lilifanyika katika sikukuu ya Bikira Maria wa Fatima ,na kuokoka kwake yeye alikuelezea ni kutokana na maombezi ya Bikira Maria.
Katika ziara zake katika nchi mbalimbali duniani,Papa amekuwa akisisitiza Ibada kwa Bikira Maria kwa kugawa zawadi ya rozali kwa kila anayekutana naye;na kumtaka asali Rozali.
Akiwa nchini Tanzania katika ziara yake ya Kichunguji mnamo Septemba 1990,Baba Mtakatifu mara tu baada ya kuwasili nchini alielekea katika Kanisa la Mtakatifu Yosefu lililopo katika Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam,ambapo aliongoza sala ya Rozali kuiombea nchi hiyo  Amani na Utulivu.
Katika Barua ya Kitume inayoitwa Rosarium Virginis Mariae (Rozari ya Bikira Maria), Papa anatoa Sala ya Bikira Maria kama tafakari juu ya mafumbo ya maisha na kazi ya Kristo iwapo itasaliwa kwa uchaji na si kwa midomo tu.
Katika kuelezea uamuzi wake wa kuongeza mafumbo matano ya nuru katika Rozari ya sasa, Papa alisema kuwa, Rozari ya Bikira Maria ni kama ufupisho kamili wa Injili uliolenga kutafakari sura ya Kristo kupitia macho ya Maria na kurudiarudia Sala ya Salamu Maria.
Alisema hadi sasa mafumbo 15 ya Rozari yaani, ya Furaha, Uchungu na Utukufu, yamekosa nyakati mahususi katika maisha ya Kristo hadharani.
Kwa sababu hiyo, Baba Mtakatifu alipendekeza kuingiza Mafumbo ya Huduma ya Kristo ya hadharani kati ya Ubatizo wake na mateso yake.
Katika Kifungu cha 21 cha barua hiyo, Papa anatilia mkazo juu ya Mafumbo ya Nuru  ya maisha ya hadharani ya Yesu na kufafanua fumbo ambalo Mkristo hutafakari katika kifungu cha matini.
Anayataja matini hayo kuwa ni Ubatizo wa Yesu, Kujidhihirisha kwake katika Harusi ya Kana, Utangazaji wake wa Ufalme wa Mungu, Mwito wake kwa uongofu, kugeuka kwake sura na kuweka Sakramenti ya Ekaristi kama kielelezo cha Fumbo la Pasaka.
Akizungumza hivi karibuni, Baba Mtakatifu alisema, “Kama kila sala ya dhati, Rozari haituondoi kutoka uhalisia wa mambo, ila hutusaidia kuiishi sala hiyo tukiwa tumeunganika na Kristo kwa ndani, huku tukitoa ushuhuda  kwa upendo.”
Papa Yohane Paulo wa Pili, pia aliwakumbusha waamini, kama alivyofanya katika barua yake ya kitume, kwamba amani na familia ni malengo mawili ya msingi ya kusali Rozari.
Kwa namna ya pekee, Papa alitoa wito wa kuwaombea watu wa Urusi ambao katika siku hizi za hivi karibuni, wamekuwa katika mateso makali wakati wa mgogoro wa utekaji nyara katika jumba la maigizo jijini Moscow.
Mgogoro huo uliisha Jumamosi ya Novemba 26, mwaka huu, baada ya makomandoo wa Jeshi la Urusi kuwaokoa mateka ambapo watekaji nyara wote 50 waliuawa pamoja na mateka 117.
“Wakati tunawaombea wahanga wa kisa hicho cha maumivu, tumwombe Bikira Mtakatifu ili matukio kama haya yasiweze kurudiwa,” alisema Papa.

No comments:

Post a Comment