Hivi
karibuni, katika maadhimisho ya Siku ya Haki Msingi za Binadamu
Kimataifa, Ubalozi wa Ufaransa nchini Benin, umewatunukia tuzo watawa wa
Shirika la Wafranciskani wanaotekeleza utume wao nchini Benin kwa
kusimama kidete kulinda, kutetea na kudumisha Injili ya Uhai kwa kuokoa
maisha ya watoto ambao hawajazaliwa, kwani hii ni haki yao msingi!
Ubalozi wa Ufaransa unawapongeza na kuwataka watawa hawa kuendelea kutekeleza dhamana hii nyeti bila kukata tamaa wala kuyumbishwa na walimwengu, kwani huu ni wajibu wao msingi. Kwa miaka mingi, Watawa hawa wamekuwa mstari wa mbele kupinga mila na desturi zilizopitwa na wakati, kwa kuwatoa watoto wadogo kama kafara, pale wanapozaliwa huku wakiwa na kasoro katika miili yao. Kila mtoto ana haki ya kuzaliwa na kuishi kama watoto wengine kwani hii ni haki yake msingi!
Umefika wakati kwa watu kuachana na mila na tamaduni zilizopitwa na wakati kwa ajili ya kutafuta utajiri, madaraka na bahati katika maisha! Maisha bora yanapatikana kwa kufanya kazi kwa juhudi, maarifa, nidhamu na weledi na kwamba, hakuna njia ya mkato katika maisha!
Ubalozi wa Ufaransa unawapongeza na kuwataka watawa hawa kuendelea kutekeleza dhamana hii nyeti bila kukata tamaa wala kuyumbishwa na walimwengu, kwani huu ni wajibu wao msingi. Kwa miaka mingi, Watawa hawa wamekuwa mstari wa mbele kupinga mila na desturi zilizopitwa na wakati, kwa kuwatoa watoto wadogo kama kafara, pale wanapozaliwa huku wakiwa na kasoro katika miili yao. Kila mtoto ana haki ya kuzaliwa na kuishi kama watoto wengine kwani hii ni haki yake msingi!
Umefika wakati kwa watu kuachana na mila na tamaduni zilizopitwa na wakati kwa ajili ya kutafuta utajiri, madaraka na bahati katika maisha! Maisha bora yanapatikana kwa kufanya kazi kwa juhudi, maarifa, nidhamu na weledi na kwamba, hakuna njia ya mkato katika maisha!
Habari kwa hisani ya Radio Vatican
No comments:
Post a Comment