Ni matumaini ya Jumuiya ya Mtakatifu Egidio kwamba, Serikali ya Tanzania pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama vitaendelea kuwa makini zaidi ili kusitisha vitendo ambavyo vinahatarisha uhuru wa kuabudu, amani, utulivu, upendo na mshikamano wa kitaifa, tunu msingi katika mchakato wa maendeleo endelevu.
Jumuiya ya Mtakatifu Egidio ina wanachama wake ambao wengi wao ni wanafunzi wa vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu ambao hukutanika kwa ajili ya kusali, kutafakari Neno la Mungu pamoja na kutoa huduma kwa maskini na wahitaji zaidi katika mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Dodoma, Morogoro na Iringa.
Jumuiya ya Mtakatifu Egidio iko pia mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi kwa njia ya mradi wake ujulikanao kama "The Dream", unaotekelezwa USA River, Jimbo kuu la Arusha, Iringa na Masanga.
SOURCE :http://sw.radiovaticana.va/news/2013/05/07/watu_wenye_mapenzi_mema_watuma_salam_kwa_wahanga_wa_shambulio_l/kws-689769
No comments:
Post a Comment